Njia Ya Uzima

Scheduled on

Saturday 20:00 21:00
Saturday 20:00 20:00

NJIA YA UZIMA


Njia Ya Uzima (Path to Life)


Ni kipindi cha neno la Mungu chenye lengo la kuwafikia watu wote wanaosikia na kuelewa lugha ya kiswahili popote duniani. Kipindi hiki kimesheheni Nyimbo za injili ,Neno la Mungu, shuhuda, madokezo ya muhimu kuhusu ufalme wa Mungu, maombi na maombezi na mambo mengi ya kukujenga katika kuishi maisha sawasawa na mapenzi ya Mungu. Kipindi kimeandaliwa na huduma ya eChurch Global kwa msaada wa Roho Mtakatifu. Makao makuu ya huduma ni Stjørdal Norway.

Huduma ya eChurch Global ni huduma ya kupeleka injili (Habari Njema) mpaka kiganjani kwako kwa njia ya mtandao. Msingi wetu umejengwa kupitia (Mathayo 28 : 19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu) . Baadhi ya majukwaa ya mitandao tunayotumia ni YouTube, Facebook, Instagram na Twitter jina ni ¨eChurch Global¨

Huduma pia inahudumia watu mbalimbali wenye uhitaji kama yatima, wajane, wagane, watoto wa mitaani nchini Tanzania n.k. Pia huduma inasaidia kwa hali na mali watumishi wengine katika kupeleka injili ya Yesu vijijini (Tanzania)

Unaweza kushiriki nasi baraka hizi kwa sadaka yako na tunakukaribisha kujiunga nasi (Tuna kikundi cha whatsapp kinaitwa Friends and Partners of eChurch Global mlango uko wazi kwajili yako pia)

Karibu wasiliana nasi kupitia:  echurch.global@gmail.com

Lead Minister, Richard Rwechungura, PhD

Whatsapp +4791706974 au +255656566534 au +255757564612 au +4792055506 au +255674698865

MEDIA Links

YouTube: https://www.youtube.com/channel/UC14uzUMtLnro3BOdS11blKQ/videos

Facebook: https://www.facebook.com/E-Church-Global-110100870547460

Instagram: https://www.instagram.com/echurch_global/

Twitter: https://twitter.com/EchurchGlobal


Read more

Podcast of previous episodes

Sorry, there is nothing for the moment.

Related news

Sorry, there is nothing for the moment.

Radio Rehoboth

107.2 FM Norway

Current track

Title

Artist

Background